Posts

Showing posts from August 29, 2013

Star Michael Scolfield (Wentworth Miller) Atangaza kuwa yeye ni shoga

Image
Star huyu mwenye miaka 41aliejipatia umaarufu kupitia tamthilia ya Prison breaka hapo jana alitangaza kuwa yeye ni shoga, kwa mujibu wa website moja, Michael aliweka wazi baada ya kukataa mualiko wa tamasha la filamu la St. Petersburg nchini Urusi kwa kile alichodai mashoga wanadharauliwa na hawatendewi haki nchini Urusi.

TUNDA MAN AAMBULIA AIBU KUTOKANA NA KESI YA MADAI YA LAKI NANE

Image
Taarifa tulizozipata ni kuwa Tunda man alikopa pesa kwa Mwanadada mmoja ambae hakupenda jina lake liwekwe mtandaoni kiasi cha laki nane kwa maelewano atamlipa baada ya muda kupita. Akizungumza na Kituo kimoja cha radio dada huyo anadai baada ya muda kupita ikabidi antafute Tunda Man ili amkumbushe madai anayomdai, lakini haikuwa kama yule dada alivyotegemea kwani aliambulia matusi, na wakati mwingine akijaribu kumpigia Tunda simu haipokelewi, ndipo dada huyo alipoamua kwenda polisi ili afungue kesi ya madai Baadae Tunda alitafutwa ndipo akakubali kuwa atamlipa kwa awamu tatu na awamu ya kwanza ilikuwa tarehe 12/08/2013 lakini tunda hakutokea kulipa deni japo waliandika makubaliano Baada ya kuona kimya japo waikubaliana ndipo maaskari polisi walipoamua kwenda nyumbani kwa Tunda man ili kumkamata lakini hawakufanikiwa kwani Tunda aliwaona na akaamua kukimbia

WABUNGEWAMCHACHAMALIA WAZIRI Mh. WILLIAM LUKUVI KUTAJA WAHUSIKA WA DAWA ZA KULEVYA

Image
.   Kauli ya waziri wa nchi ofisi ya waziri Mkuu Sera,Uratibu na Bunge Mh. William lukuvi ya "hakuna mbunge hata mmoja atakayesalia salama endapo serikali itayataja majina ya watu wanaotajwa kuhusika katika biashara ya dawa za kulevya" imechukua  sura mpya baada ya baadhi ya wabunge kumtaka kuyataja majina hayo bungeni au kuifuta kauli yake. Kauli iliyowafanya baadhi ya wabunge kutopata usingizi na kumfanya mbunge Simanjiro Mh christopher Ole Sendeka kuomba muongozo wa spika chini ya kanuni ya 68 saba kwa madai kuwa kauli hiyo si tu inalidhalilisha bunge bali pia wabunge hao watakosa sehemu za kuficha nyuso zao kwa wale ambao hawafahamu hata namna dawa hizo zinavyofanana. Baada ya kuuomba uongozo huo,naibu spika wa bunge la jamhuri ya muungano wa tanzania mh job ndugai akatoa fursa kwa waziri husika kutoa maelezo ambapo licha ya kukiri kulijibu swali hilo ameongeza kuwa serikali hii inayoongozwa kwa misingi ya sharia kamwe haitakubali kutangaza

LUDWIGNCHEMBA ATAKA MBOWE NA DR. SLAA WAKAMATWE KWA MAUAJI YA RAIA

Image
 MBUNGE wa Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba (CCM), amechafua hali ya hewa bungeni kwa kuitaka Serikali kuwachukuliwa hatua viongozi wa juu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Mbunge huyo alisema mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe pamoja na Katibu Mkuu wake, Dk. Wilbroad Slaa, wanapaswa kuchukuliwa hatua kwa madai ya kusababisha mauaji ya raia. Mwigulu, ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bara, alisema katika kipindi cha miaka miwili tangu nchi ilipotoka kwenye uchaguzi, viongozi hao wamekuwa wakihamasisha maandamano na kusababisha umwagaji wa damu za Watanzania. “Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi cha miaka miwili tangu nchi yetu ilipomaliza Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010, Mbowe na Dk. Slaa wamekuwa wakitoa kauli za wazi na hata kusababisha mauaji ya watu bila hatia. “Kutokana na hali hii, sijui Serikali inafanya nini katika kuwachukulia hatua, kwani viongozi hawa wamekuwa wakitafuta umaarufu wa kisiasa kwa kuchoche

BASI LA HOOD LAUA MTU MMOJA NA KUJERUHI 15

Image
Mtu mmoja amefariki dunia na 15  wamejeruhiwa baada ya basi  la Kampuni ya Hood  likitokea kilombero kwenda jijini  Dar es salaam kumgonga  mtembea kwa miguu na kisha kuacha njia na kupinduka katika eneo la Kiembeni  Mikese Mkoani  Morogoro.    Mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Morogoro  Bonifasi Mbao  akizungumza kwenye  eneo la tukio amesema chanzo cha ajali  hiyo ni mwendo kasi ambapo dereva wa basi  gari  ilimshinda na kugonga mtembea kwa miguu na kisha kupinduka ambapo  dereva wa basi amekimbia mara baada ya tukio la ajali...   Taarifa za  madaktari  katika hospitali ya Mkoa wa Morogoro  zimeeleza  majeruhi wanaendelea na matibabu na mwili wa marehemu umehifahiwa katika chumba cha maiti hospitali ya mkoa wa morogoro .

VIJI MAMBO VYA KWENYE SIMU

Image
Mrembo alipokea simu ngeni na mambo yalikuwa kama hivi: Simu: Hellow una boy friend? Mrembo: Ndio nine. Kwani we nani? Simu: Mimi baba yako. Kumbe una boy friend ukirudi utanitambua. Simu ikakatika akiwa na mawazo nini afanye. Simu ikaita tena kwa namba ngeni. Simu: Hello una boy friend? Mrembo: Hapana sina! Simu: Vipi mpenzi ina maana unanisaliti? Mrembo: Hapana BABY nilijua baba! Simu: Ni mimi baba yako nilitaka kuhakikisha tu kama kweli una boy friend. UTANIKOMA LEO