Posts

Showing posts from August 7, 2013

MADAM RITA AFUNGUKA KWA SABABU ZILIZOMFANYA AIHAMISHIE BONGO STAR SEARCH TBC 1

Image
  Epiq Bongo Star Search ya mwaka 2013 haitaoneshwa tena kupitia ITV. Mwaka huu shindano hilo la kusaka vipaji vya kuimba litakuwa likioneshwa kupitia TBC1.  Kupitia Facebook, Rita Paulsen aka Madam Rita ambaye ni mwanzilishi na jaji mkuu wa shindano hilo ametoa sababu mbili za kuhamisha matangazo hayo kutoka ITV hadi TBC1. “Baada ya kusoma maoni yenu, ningependa kufafanua sababu mbili za kurusha Epiq Bongo Star Search 2013 kupitia kituo cha Televisheni cha TBC1.  Kwanza kabisa ni sababu za kibiashara ndio zimepelekea kipindi cha EBSS kurushwa kupitia TBC1 na sababu ya pili ni kwamba baada ya kwenda kidigitali, TBC1 sasa inapatikana kwenye ving’amuzi karibia vyote vikiwemo Star Times, DSTV na Zuku.”Ila kwa wawle wanao tumia madishi au mfumo wa analogia watashindwa kuona mzshindano aya mwaka kupitia kubadilisha utalatibu wa kurusha kipindi cha Epiq Bongo star search