Posts

Showing posts from August 30, 2013

RAIS KIKWETE AMUOMBA RAIS WA UGANDA AONGEE NA KAGAME ILI KUMALIZA UGOMVI ULIPO

Image
RAIS Jakaya Kikwete, amewasiliana na Rais wa Uganda, Yoweri Museveni, ili azungumze na Rais wa Rwanda, Paul Kagame kwa nia ya kumaliza mvutano wa maneno kati yao kwa busara.   Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alisema hayo jana bungeni, alipokuwa akijibu swali la Kiongozi wa Upinzani bungeni, Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe (Chadema).   “Tunataka suala hili limalizike kwa njia ya busara, ili watu waendelee kuchapa kazi, ninaamini busara zitatumika kumaliza tatizo hilo,” alisema. Akiuliza swali katika kipindi cha maswali ya Papo kwa Hapo kwa Waziri Mkuu jana, Mbowe alitaka kujua kauli ya Serikali na mikakati iliyopo kupata suluhu katika mvutano wa maneno uliojitokeza kati ya Rais Kikwete na Rais Kagame.   Pia Mbowe alitaka Serikali kuunda jopo la ushawishi wa kimataifa, kutokana na Rwanda kuonekana kushawishi nchi za Uganda na Kenya, jambo ambalo linaashiria kuitenga Tanzania katika shughuli mbalimbali za Jumuiya ya Afrika Mashariki.   Kwa mujibu wa Mbowe, k

"SINA MPANGO WA KUACHANA NA DIAMOND NA SIJAONA MWANAUME KAMA YEYE"....PENNY

Image
Baada ya hivi karibuni kuandikwa habari iliyoeleza kwamba nchini Kenya kuna demu aliyemzimikia ile mbaya mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond’ huku akiahidi kumpa penzi zito, mpenzi wa msanii huyo Peniel Mwingilwa ‘Penny’ ameibuka na kudai hatishwi na maneno hayo. Akizungumza na mwandishi wetu hivi karibuni, Penny ambaye sasa anapika na kupakuwa kwa Diamond alisema anamuamini sana mpenzi wake huyo na kwamba kuhusishwa kwake na mambo ya mademu kila kukicha kunatokana na kazi yake. “Yatasemwa mengi lakini siwezi kumuacha Diamond, namuamini na najua haya yote yanayotokea ni kwa sababu ya kazi yake kwa hiyo wanaodhani mimi nitayachukua na kuamua kumuacha watasubiri sana, ndiyo kwanza penzi letu linazidi kushamiri,” alisema Penny.

RAY C AMUA KUMPOKEA BWANA KUWA MWOKOZI WA MAISHA YAKE RASMI,BAADA YA KUBATIZWA

Image
  rayc1982 Nimebatizwa Rasmi Leo kanisa la Siloam...Shika neno tenda neno,Shetani huna nafasi tena kwenye Maisha yangu,nimepewa ruksa na Mwenyez Mungu nikukanyage kanyage Usinizoee!!!!Ameeeen!