Posts

Showing posts from September 8, 2013

JINSI FIESTA 2013 ILIVYOKUWA JIJINI MBEYA SOKOINE WALIVYO JITOKEZA

Image
Msanii wa muziki wa kizazi kipya,ambaye kwa sasa anafanya vyema kwenye anga za muziki huo,Neylee akiimba kwa hisi jukwaani huu wakati tamasha la Serengeti Fiesta likiendelea kwa shangwe ndani ya uwanja wa Sokonine. Wakazi wa jiji la Mbeya wakiwa wamejitokeza kwa wingi usiku huu kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2013 ndani ya uwanja wa Sokoine,ndio kwanza shoo inaanza ambapo msanii aliyewahi kuiwakilisa shindano la BSS,Walter Chilambo ndiye aliyefungua pazia la onesho hilo usiku huu.   Tamasha la Serengeti Fiesta 2013 likiendelea usiku huu kwenye uwanja wa Sokoine,Mkoani Mbeya  Mama wa miduara ya Kibongofleva,Shilole akiwa na madensa wake wakitumbuiza jukwaani usiku huu ndani ya tamasha la Serengeti fiesta 2013,ndani ya uwanja wa Sokoine mkoani Mbeya.  Sehemu ya umati wa watu. Mkali mwingine wa hip hop (bongofleva),Ney wa Mitego akikamua jukwaani usiku huu ndani ya tamasha la Serengeti Fiesta 2013,kwenye uwanja wa Sokoine,mjini Mbeya.  Wakaz

KWANINI ROBIN VAN PERSIE HAJAPIGA HATA SHUTI MOJA GOLINI KATIKA MECHI DHIDI YA LIVERPOOL NA CHELSEA?

Image
Robin van Persie alikuwa kwenye kiwango kizuri dhidi ya Swansea katika mchezo wa ufunguzi wa msimu. Mshambuliaji huyo wa kidachi alionekana ameuanza msimu kama alivyoumaliza uliopita akiwa kwenye fomu nzuri. Pamoja na kufunga mabao mawili katika mechi ya kwanza, van Persie ameshindwa kupiga hata shuti moja lilolenga goli katika michezo miwili iliyopita - mechi ambazo Manchester United ilifeli kufunga bao hata moja.  Kiwango cha van Persie kwa ujumla katika mechi mbili zilizopita. Okay! kama tulivyoona kwamba RVP hakupiga mpira wowote uliolenga goli huku wastani wake wa kupiga mipira ukipungua mpaka  33%. Dhidi ya Liverpool,mambo yakawa mabaya zaidi huku akipoteza nafasi mbili kwa kupiga mipira nje huku jaribio lake la 3 likizuiwa na walinzi wa lango la Liverpool.  Sio tu kwamba alionekana kutokuwa mchezoni pia alikosa ideas kabisa mbele ya lango (kwa ubora wake) lakini pia mchango wake kwenye umekuwa wa chini sana. Namba ya pasi kwa mchezo imekuwa ikipungua