“Tunataka kuwaambia Watanzania kuwa klabu yetu ni mpya na ina falsafa mpya kabisa, vijana n dio msingi wetu. Pia tunajua mashabiki ni mchezaji wa 12, tunawaomba wajitokeza leo kwa wingi kwani tutawapa raha kama tulivyofanya huko nyuma”. Alisema Maka. WAKALI wapya wa ligi kuu soka Tanzania bara `Nyuki wa nyanda za juu kusini`, klabu ya Mbeya City wametamba kuwa leo wanataka kuisimamisha nchi kwa muda na kuwajulisha watanzania kuwa falsafa yao mpya na mtazamo mpya kweli unafanya kazi. Akizungumza kwa njia ya simu kutoka jijini Mbeya na mtandao wa Samwelmlawa muda mfupi uliopita, Kocha msaidizi wa klabu hiyo, Maka Mwalwisyi amesema wachezaji wote wana morali kubwa na wanategemea kuiambia Tanzania kuwa falsafa mpya imekuja na watapa matokeo mazuri jioni ya leo dhidi ya JKT Ruvu na kuongoza ligi kwa saa kadhaa. “Falsafa na mtazamo mpya ndio dira yetu, sisi tunaamini kuwatumia vijana wadogo, tunawa