Posts

Showing posts from September 28, 2013

JITAMBUE:UHUSIANO KATI YA MAPENZI NA HOFU.

Image
SAYANSI ya mapenzi inakataa kuwepo mapenzi ya kweli sambamba na hofu. Mtu hawezi kusema anampenda mwenzake wakati kuna vitu anaviogopa kutoka kwa mpenzi wake kiasi cha kumuondolea ujasiri. Ifahamike kwamba, ukamilifu wa mapenzi kwa   ni namna hofu inavyoweza kushughulikiwa na kuondoshwa kabisa miongoni mwa wapendanao. Uchunguzi unaonyesha kwamba, woga umekuwa sumu kubwa ya mapenzi na mara nyingi imebainika kwamba, kila woga unavyozidi kumwingia mtu ndivyo anavyopoteza mshawasha wa kupenda. Tunafahamu ubora wa majiko ya gesi lakini wengi wamekuwa hawataki kuyatumia kwa sababu wanaogopa kulipukiwa, hivyo kuamua bora watumie kuni, mkaa au mafuta ya taa ambayo wanaamini ni salama. Hii ina maana kwamba, mwanamke au mwanaume anaweza kuwa tayari...

MAGAZETI YA MWANANCHI NA MTANZANIA YAFUNGIWA

Image
Serikali imeyafungia kutochapishwa Magazeti ya MWANANCHI na MTANZANIA kuanzia 27 Septemba, 2013 kutokana na mwenendo wa magazeti hayo kuandika habari na makala za uchochezi na uhasama kwa nia ya kusababisha wananchi wakose imani kwa vyombo vya dola hivyo kuhatarisha amani na mshikamano uliopo nchini...

ROSE NDAUKA SASA KUZAA BILA NDOA

Image
Staa wa filamu za Bongowood, Rose Ndauka ambaye ni mjamzito anadaiwa kuwa atazaa kabla ndoa mwezi Aprili, mwakani. Akizungumza na mwanahabari wetu, mchumbaa’ke, Malick Bandawe ambaye ni memba wa kundi la muziki la TNG alianika aya za Kurani kuwa katika Dini ya Kiislamu si ruhusa kufunga ndoa na mwanamke ambaye ni mjamzito kwani ni sawa na kufunga ndoa na watu wawili hivyo anamsubiri ajifungue kwanza. “Ni kweli mchumbaa

BABU WA LOLIONDO TENA!

Image
Ambilikile Mwaisapila ‘Babu wa Loliondo’. : MCHUNGAJI mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ambilikile Mwaisapila ‘Babu wa Loliondo’ amesema Mungu ameendelea kujifunua kwake na kumuonesha kuwa Tanzania itakuwa kioo cha Afrika na baadaye kioo cha dunia. Ametoa kauli hiyo Septemba 24, mwaka huu mbele ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda wakati akizungumza na wakazi wa Kijiji cha Samunge, wilayani Ngorongoro mkoani Arusha wakati msafara wa Waziri Mkuu uliposimama nyumbani kwake ili kumsalimia akiwa njiani kurejea mjini Arusha. Mchungaji Mstaafu Mwaisapila aliyesifika kwa tiba ya kikombe cha dawa, alisema kuna mambo mengi ambayo..

Picha ya msanii RECHO akiwa katika pozi la NUSU UCHI

Image
MSANII wa filamu za kibongo, Rachel Haule ‘Recho’ hivi karibuni aligeuka kituko baada ya kutupia picha ya nusu utupu katika mtandao wa kijamii. Picha hiyo ambayo Recho amevaa shati tupu (inayoonesha ndani) bila kuvaa kitu kingine chochote, aliitupia kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram ambapo mashabiki na marafiki zake walichangia huku wakimlaumu kuwa hakufanya vizuri kuiweka picha hiyo ya aibu mtandaoni. Mwandishi  wetu alimuuliza...

Ulimboka, Costa na Pawasa wachambua uchezaji Simba

Image
WACHEZAJI waliojijengea heshima kubwa wakati wakiichezea Simba wametamka maneno ya moyoni kuhusiana na mwenendo wa timu hiyo. Wachezaji hao ni Boniface Pawasa, Victor Costa, Selemani Matola na Ulimboka Mwakingwe lakini kocha Talib Hilal alipowasikia naye akaongeza neno. Pawasa ambaye alikuwa beki kisiki alisema: “Kikosi bado kinahitaji kurekebishwa hasa kwenye kombinesheni ya mabeki na ushambuliaji bado hapako sawa sana. Nafikiri baada ya mwaka Simba wanaweza kuwa kwenye ubora, wakizingatia misingi ya usajili, watu muhimu wakae sehemu muhimu.” Victor Costa ambaye pia ni beki alisema: “Simba ya..

YANGA VS RUVU SHOOTING: MRISHO NGASSA KUIBEBA AMA KUIPONZA YANGA?

Image
Yanga ina zaidi ya mwezi bila kushinda mechi yoyote. Sare nne mfululizo zilizokuwa zikionekana matope ziligeuka nafuu baada ya kipigo kutoka kwa Azam kilichowafanya wajikute wakiambulia pointi sita tu kati ya kumi na tano katika mechi tano za msimu mpya wa ligi kuu. Gumzo kubwa kuelekea pambano la leo ni kurudi dimbani kwa Mrisho Ngassa. Ngassa anarudi Jangwani kwa mara ya Kwanza baada ya kuwa 'utumwani' Azam na Simba kwa misimu mitatu iliyopita. Anarudi uwanjani baada ya kutumikia adhabu ya mechi sita kwa kusajili timu mbili, Simba na Yanga. Macho na masikio yatakuwa kwake hasa baada ya kugonga vichwa vya habari kwa takriban wiki nzima kuelekea pambano la leo. Unaweza kufananisha sakata lake na lile la Liverpool na Suarez.