Posts

Showing posts from July 12, 2013

ujio mpya wa Afande Sele akipewa sakoti na Belle 9 Dini Tumeletewa

JESHI LA POLISI LATEUA ASKARI WA KUMFUATA AGNESS MASOGANGE ALIYENASWA NA MADAWA YA KULEVYA AFRIKA KUSINI

Image
Jeshi la Polisi litapeleka askari wake Afrika Kusini kuwahoji washiriki wa video za wasanii wa muziki wa Bongo fleva, Agnes Gerald ‘Masogange’ na mwenzake Melisa Edward waliokamatwa nchini humo na dawa za kulevya. Kamanda wa Kikosi cha Kuzuia Dawa za Kulevya, Godfrey Nzowa aliiambia  Mwananchi  kwa simu jana kuwa watawapeleka polisi kuwahoji na wanaamini wahusika watawaeleza wahusika wa mzigo huo. Wasichana hao walikamatwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Oliver Tambo nchini Afrika Kusini wakitokea Tanzania wakiwa na kilo 150 za dawa za kulevya aina ya Crystal Methamphetamine. “Tutawapeleka askari wetu kuwahoji, tumekwishaanza uchunguzi wa hili...wote watakaohusika katika hili tutawakamata, lakini tunakwenda polepole hatua kwa hatua kuhakikisha tunawanasa wahusika sahihi,” alisema Nzowa. Naye Mkurugenzi wa Uwanja wa Ndege wa Juliu