Posts

Showing posts from September 13, 2013
Image
YANGA WAPEWA SIKU 14 KUWALIPA NSAJIGWA NA MWASIKA DENI LAO LA MILLIONI 15.5 Yanga imepewa siku 14 kuanzia leo (Septemba 13 mwaka huu) kuwalipa waliokuwa wachezaji wake msimu uliopita, nahodha Shadrack Nsajigwa na Stephen Mwasika wanaoidai klabu hiyo jumla ya..............

VATICAN SASA KUJADILI KUHUSU UWEZEKANO WA MAPADRI WAKATOLIKI KUOA..!!

Image
Waziri wa Mambo ya Nje wa Vatican, Askofu Mkuu Pietro Parolin . Suala la mapadri wa Kanisa Katoliki kuoa au la, limeibuka upya na tayari limeanza kuzua mijadala mikali duniani. Mjadala wa sasa umeibuliwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Vatican, Askofu Mkuu Pietro Parolin ambaye aliteuliwa hivi karibuni kushika wadhifa huo aliposema useja, yaani maisha ya utumishi ndani ya kanisa bila ndoa siyo imani, bali utamaduni na mazoea. Akizungumzia kauli hiyo, Msemaji wa Vatican, Federico Lombardi alisema kauli ya Askofu Parolin haipingani na mafundisho ya kanisa. Askofu Mkuu Parolin ambaye aliteuliwa karibuni na Papa Francis kushika wadhifa huo kutoka kwa Kardinali Tarcisio Bertone amenukuliwa na Gazeti la El Universal la Venezuela, Amerika ya Kati akieleza kuwa suala hilo linaweza kujadiliwa.

BAADA YA KUTWAA UBINGWA WA DUNIA SERIKALI KUMJENGEA NYUMBA YA KISASA FRANCIS CHEKA

Image
Serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania kupitia mkuu wa mkoa wa Morogoro leo hii imemfanyia hafla fupi ya kumpongeza Bondia Francis Cheka aliyeiletea sifa kubwa nchi baada ya kushinda ubingwa wa dunia kwa kumtandika aliyekuwa bingwa wa dunia Phil Williams kutoka nchini Marekani.

ALIYEKUWA MISS TANZANIA 2006 AFUNGUKA SIFA 4 WANAUME WANAO MMEZEA MATE:

Image
 MREMBO anayefanya vizuri katika mambo mengi nchini, Jokate Urban Mwegelo (pichani) ametaja sababu nne zinazowafanya wanaume kumzimikia, akiwemo nyota wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’.  Akiandika katika mtandao wake wa Kidoti Life Style, Jokate, mshindi wa pili wa Miss Tanzania 2006, alizitaja sababu hizo kuwa ni kujiamini, kujitegemea, kupendeza na tabasamu muda wote.

TUNDU LISU..AKATAA UAMUZI ULIOTOLEWA NA CCM KUTAKA KUIFUTA KESI YAKE:

Image
  WAKATI viongozi mbalimbali wa CHADEMA wakiwasili mjini Dodoma kuungana na Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, katika rufaa ya kupinga ubunge wake inayoanza kusikilizwa leo, mbunge huyo amekataa uamuzi CCM kutaka kuifuta kesi hiyo. Juzi CCM kupitia kwa wakili wake, Godfrey Wasonga, iliwasilisha barua katika Mahakama ya Rufaa Dodoma na nakala kwa Lissu ikiomba mahakama hiyo kuifuta kesi hiyo.     Kwa mujibu wa wakili huyo, sababu ya kuomba kufutwa kwa kesi hiyo ni walalamikaji wote kujitoa na kuapa mahakamani kuwa hawakuwa tayari kuendelea na kesi hiyo.