Posts

Showing posts from October 18, 2013

VITA YA WATANI WA JADI J'PILI

Image
KESHOKUTWA Jumapili litapatikana jibu la nani mbabe katika mechi ya kwanza ya Ligi Kuu Bara ambayo itawakutanisha watani wa jadi, msimu huu. Simba watakuwa wenyeji wa Yanga, kila upande utakuwa unacheza mechi yake ya tisa ya ligi hiyo msimu huu, huku mabingwa watetezi wakionekana kupania kupanda na Simba kutaka kujichimbia zaidi kileleni. Simba ina pointi 18 kileleni wakati Yanga ina 15 katika nafasi ya nne, iwapo Simba itateleza basi zitalingana pointi. Takwimu zinaonyesha Simba inafanya vizuri zaidi hadi sasa lakini zile za uzoefu wa mechi za watani, Yanga wanaonekana kuwa na kikosi imara zaidi. Inaonyesha lazima ‘mtu atakaa’, lakini si rahisi kung’amua ni yupi.

SIMULIZI YA MAJONZI

Image
Stori: HARUNI SANCHAWA NA MAKONGORO OGING’ KUNA simulizi ya majonzi nyuma ya kifo cha mwanamke Lewina  Kinemo (38) aliyedaiwa kujirusha ghorofani katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dar es Salaam ambako alikwenda kujifungua, Risasi Jumamosi lina mkasa mzima. Lewina alifariki dunia Jumanne iliyopita saa tano na dakika arobaini alipokuwa anatoka kumnyonyesha mwanaye aliyezaliwa wiki moja nyuma. MWANAMKE ALIYEKUWA NA MAREHEMU Kwa mujibu wa mwanamke aliyekuwa na Lewina (jina halikupatikana mara moja) muda mfupi kabla ya kifo, marehemu alifanya mambo yenye viashiria vya kifo chake na hajui nini kilimtokea