Posts

Showing posts from September 7, 2013

Sakata la mwanafunzi wa KIDATO CHA NNE aliyezalishwa na msanii DIAMOND

Image
MREMBO aliyetimuliwa shule akiwa kidato cha nne baada ya kutundikwa mimba, Sasha Juma ameibuka na madai kuwa amezaa na staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’. MCHEZO MZIMA Habari kutoka kwa chanzo chetu cha kuaminika zilidai kuwa Sasha na Diamond walikutana katika mgahawa mmoja uliopo kwenye maduka ya Mlimani City, Dar na ndipo walipoanzisha uhusiano. Ilidaiwa kuwa Sasha akiwa na marafiki zake alitoka kwenye moja ya maduka hayo ambapo alimkuta Diamond na binamu yake, Romy Jones wakiwa wamekaa nje ya mgahawa huo. Ilidaiwa kwamba kwa kuwa Sasha anajuana na Romy muda mrefu, aliwafuata kisha akawasalimia ndipo Diamond akaonekana kuvutiwa na mrembo huyo na kumwambia kuwa atachukua namba yake ya simu ya kutoka kwa Romy kwa vile alikuwa nayo. Chanzo chetu hicho kilizidi kutiririka kuwa baada ya hapo Sasha aliondoka na marafiki zake, kipindi hicho akiwa anasoma kidato cha nne katika Shule ya

WAKAZI WA MBEYA WAJITOKEZA KWA WINGI KWENYE FURSA YA VIJANA NDANI YA TEKU.

Image
 Sehemu ya vijana waliojitokeza kwa wingi kwenye semina hiyo ya Fursa kwa vijana wakifuatilia mijadala mbalimbali iliyokuwa ikijadiliwa ukumbini humo. Muwakilishi wa NSSF-Makao Makuu Bwa,Salim Khalfan akizungumza mbele ya vijana mbalimbali waliojitokeza kwenye semina ya Fursa kwa vijana,iliofanyika mapema leo   kwenye ukumbi wa   chuo cha Teofilo Kisanji kilichopo maeneo ya Block T-Mama John mkoani Mbeya.   Semina hiyo iliyoandaliwa na Clouds Media Group,imefadhiriwa na shirika la NSSF;Zantel,MaxMalipo,Lake Oil,TPSF. Mmoja wa Vijana Wajasiliamali ,ambaye ana mradi mkubwa wa kuuza juisi,Gasto Sony mkazi Uyole mkoani Mbeya,akieleza zaidi kwa vijana wenzake waliojitokeza kwa wingi kwenye semina hiyo,namna ambayo ameweza kuitumia fursa alioipata na kuwa mjasiliamali wa kuuza juisi kisasa kabisa.   Mkurugenzi wa Masoko wa kampuni ya bia ya Serengeti,Bwa.Eprahim Mafuru akizungumza na wakazi wa Mbeya (hawapo pichani) waliojitokeza kwenye semina ya F

MBUNGE WA MBEYA MJINI MH JOSEPH MBILIMYI AJISALIMISHA POLISI BAADA YA KUTAFUTWA KWA SIKU MBILI

Image
BAADA ya Jeshi la Polisi mkoani Dodoma kumsaka kwa siku mbili bila mafanikio mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi, maarufu kama Sugu (CHADEMA), akidaiwa kumpiga na kumjeruhi mmoja wa askari wa Bunge, hatimaye alijisalimisha mwenyewe jana jioni. Taarifa zilizotufikia wakati tunakwenda mitamboni, Sugu alikwenda polisi akiongozana na Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, na wabunge Tundu Lissu (Singida Mashariki), John Mnyika (Ubungo) na Joshua Nassari (Arumeru Mashariki). Akizungumza na  mwandishi wetu, Mnyika alisema kuwa Sugu hakukamatwa bali alijipeleka mwenyewe polisi kwa hiari yake na kwamba jioni hiyo majira ya saa 1:10 alikuwa akiandikisha maelezo yake. Wakati Sugu akijisalimisha, wanasheria wa Bunge nao walikuwa wamejifungia kuangalia namna ya kumkabidhi mbunge huyo mikononi mwa sheria. Juzi na jana viwanja vya Bunge vilitawaliwa na idadi kubwa ya polisi waliotumwa kumkamata Sugu lakini mpaka Bunge linaahirishwa jioni haikujulikana ni wapi alikokuwa

VIONGOZI WA MAZIWA MAKUU WATOA SIKU TATU KWA M23 NA SERIKALI YA DRC KUREJEA MEZA YA MAZUNGUMZO.

Image
  Wapatanishi wa mgogoro wa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wametoa muda wa siku tatu kwa waasi wa M23 na serikali ya nchi hiyo kurejea kwenye meza ya mazungumzo huko jijini Kampala Uganda. Hayo ni baada ya kikao cha viongozi wa kanda ya maziwa makuu kiliyofanyika juzi huko kampala Uganda. Kiongozi wa kundi la M23 Bertrand Bisimwa amesema wao wapo tayari kwa mazungumzo na wajumbe wake wamewasili mjini Kampala kwa ajili ya mazungumzo hayo. Bertrand Bisimwa amesema kundi lake limechukua uamuzi wa kurejea katika meza ya mazungumzo wakitekeleza wito huo wa mataifa yanayounda Kanda ya Maziwa Makuu kutaka mazungumzo kuendelea ndani ya siku tatu. Mazungumzo hayo baina ya serikali ya DRC na kundi la waasi wa M23 yalianza tangu Desemba mwaka jana jijini Kampala lakini hadi sasa hayajafikia kwenye hatua ya kuridhisha. Raisi wa Uganda Yoweri Museveni ambaye ni mwenyekiti wa mkutano wa Jumuiya ya Nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu amesema kuwa kuna nafasi ku

SERIKALI YA TANZANIA IMEWATAKA KENYA,UGANGA,RWANDA WATUELEZE WALICHOZUNGUMZIA KWA SIRI

Image
Serikali imeziomba nchi za Kenya, Uganda na Rwanda kuipa taarifa ya mikutano waliyoifanya bila ya kuishirikisha hivi karibuni.  Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe akizungumzia na waandishi wa habari ofisini kwake jana alisema wameziomba nchi hizo kuitaarifu kile walichokijadili. Alisema kwakuwa nchi hizo ni miongoni mwa nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, zilitakiwa kutoa maelezo kwa Umoja huo ili kila nchi wanachama ziweze kutambua lengo lao. Membe alisema pia Serikali ya Tanzania, imeziomba nchi hizo kuwapa maelezo ya kile walichokuwa wakikijadili katika mkutano wao wa hivi karibuni uliofanyika Kenya. “Tumewaomba wenzetu hawa, kutueleza mkutano wao ulikuwa unahusu nini, kwani tulipaswa kujua kutokana na kuwa wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, hata kama hawakutaka kutushirikisha,” alisema Membe na kuongeza: “