Posts

Showing posts from September 25, 2013

Siku tatu za maombolezo zaanza nchini Kenya baada ya oparesheni dhidi ya magaidi katika jengo la Westgate kutamatika

Image
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta, akiwahutubia wananchi wa Taifa hilo REUTERS/Presidential Strategic Communications Unit Wananchi wa Kenya hii leo wameanza maombolezo ya siku tatu kama ilivyotangazwa na Rais wa nchi hiyo Uhuru Kenyatta, maombolezo hayo yanakuja baada ya kutamatika kwa opersehni nzito ya kuwakabili magaidi walioteka jengo la maduka la Westgate toka siku ya jumamosi mwishoni mwa juma lililopita.

Moyes awaomba subra mashabiki

Image
Kocha mpya wa Man U David Moyes Kocha wa Manchester United David Moyes amewaonya mashabiki wa mabingwa wa ligi kuu ya England kwamba anahitaji kuimarisha kikosi chake na kwamba kipigo cha Jumaapili ambapo walichapwa 4-1 na Manchester City huenda isiwe ndio mwisho wa matokeo kama hayo. "kutatokea siku kama ile ya Jumaapili na huenda tukakabiliwa na matokeo zaidi kama hayo kwa sababu tuko katika kipindi cha mpito," alwaaambia waandishi habari kabla ya pambano la Jumaatano la kombe la Capital One dhidi ya Liverpool...