Posts

Showing posts from September 6, 2013

KOCHA KIM PAULSEN WA TAIFA STAR AFUNGUKA NA MECHI YA GAMBIA SEPT 7 2013

Image
  Licha ya kupoteza nafasi ya kufuzu kushiriki fainali za kombe la dunia, kocha mkuu wa timu ya soka ya Taifa,  Taifa Stars Kim Paulsen amesema lengo lake ni kuona kikosi chake kinamaliza katika nafasi ya pili kwenye kundi C kwa kuifunga Gambia katika mchezo wa mwisho wa kukamilisha ratiba utakaochezwa Septemba 7 nchini humo. Stars ambayo ilianza vema michuano hiyo na kuweka hai matumaini ya kufuzu kushiriki fainali za kombe la dunia zitakazochezwa mwakani nchini Brazil kabla ya kupoteza mechi mbili dhidi ya Morroco ugenini na dhidi ya Ivory Coast hapa nyumbani na kujikuta ikiangukia katika nafasi ya tatu kwenye kundi lake linaloongozwa na tembo wa Ivory ccast na kufuatiwa na Morrocco huku Gambia ikikamata mkia. Akizungumza kwenye kambi ya timu hiyo jijini dar es salaam  Kim Paulsen amesema baada ya kupoteza nafasi ya kusonga mbele kwenye michuano ya kufuzu kombe la dunia sasa amejikita katika kutengeneza kikosi imara kwa ajili ya mashindano ya kufuzu fa

Kambi ya upinzani bungeni imesema haitaunga mkono muswada wa sheria ya marekebisho ya katiba ya mwaka 2013.

Image
  Kambi ya upinzani bungeni imesema kutokana na mtafuruku uliotokea bungeni kwa kutolewa nje kiongozi wa kambi hiyo Mh. Freeman Mbowe amesema hawaungi mkono muswada  wa sheria ya marekebisho ya katiba ya mwaka 2013 kwa kuwa  haiwatendei haki watanzania . Akizungumza katika mkutano na vyombo vya habari katika ukumbi wa Pius Msekwa bungeni mjini Dodoma kuhusiana na mtafuruku uliotokea bungeni kiongozi huyo wa kambi ya upinzai bungeni Mh Freeman Mbowe amesema hawatashiriki katika mjadala huo kwa kile walichodai kuwa chama cha mapinduzi (CCM) kina ajenda ya siri na kushiriki kwao hawatakuwa wanawatendea haki watanzania Akizungumzia juu ya kile kinachoonekana kwa sasa kuwa ni uhusiano mwema baina ya chama cha wananchi (CUF) na Chadema,mbunge wa Mkanyageni kupitia CUF  Mh Habib Mnyaa amesema siasa haina adui wala rafiki wa kudumu na hivo wameungana na Chadema katika kutetea haki,usawa na maslahi ya wananchi wa Zanzibara na wale wa Tanzania Bara Katika

MJADALA WA MUSWADA WA MABADILIKO YA SHERIA YA KATIBA WALAZIMIKA KUSIMAMA KWA MUDA LEO BAADA KUTOKEA HALI YA KULUMBANA KWA WABUNGE

Image
  Mjadala wa muswaada wa mabadiliko ya sheria ya katiba wa mwaka 2013 umeshindwa kuendelea bungeni baada ya kutokea hali ya kurushiana maneno ya kashfa,kejeli iliyosababisha kurushiana makonde baina ya baadhi ya wabunge wa kambi ya upinzani bungeni dhidi ya askari wa bunge  kufuatia amri ya naibu spika wa bunge Mh Job Ndugai kuwaamuru askari hao kumtoa nje kiongozi wa kambi ya upinzani nje  ya ukumbi wa bunge hatua iliyoonekana kupingwa na wabunge wote wa vyama vya upinzani  isipokuwa Mwenyekiti wa TLP Mh Augustine Lyatonga Mrema. Mara baada ya kipindi cha maswali na majibu ya papo kwa hapo kwa Waziri mkuu na kufuatiwa na kipindi cha maswali na majibu bungeni kwa mujibu wa ratiba ya bunge ilikuwa ni zamu ya wabunge kuendelea kuchangia muswaada wa marekebisho ya sheria ya katiba wa mwaka 2013. Hata hivyo baadhi ya wabunge wakasimama na kuomba muongozo wa spika wakiitaka serikali kuuondoa muswaada huo bungeni kwa ajili ya kurekebisha  mapungufu ka