Posts

Showing posts from August 3, 2013

UJIO WA TOFAUTI WA MWANAMUZIKI NAY WA MITEGO KUTOA MAKAVU KWA ZITO KABWE

Image
Mfalme wa kudiss Tanzania, Nay wa Mitego amerejea tena kuchafua hali ya hewa kwa kutengeneza mijadala kwenye radio na kwenye mtandao kwa ngoma yake mpya, Salam Zao. Kwenye Salam Zao, Nay ameendeela kufanya kile akifanyacho kwa uzuri (do what he does best) kuponda.   Awamu hii list ya aliowadiss imeongezeka zaidi na kuingia pia kwenye siasa huku akiendelea kuwapa madongo wana hip hop wenzie. Ameanza kwa kumdiss Madee kwa kusema kuwa yeye ndio rais wa Manzese na kwamba Madee amesanda. “Mi ndo rais wa Manzese yule tozi kasanda, Manzese mikono juu naiongoza kamanda,” anachana Nay. Nay wa Mitego ameendelea kuwadiss wana hip hip huku akiijita kuwa yeye ndio gangster rapper na anatengeneza hela huku wengine wakinuka vikwapa. Hakusita pia kuwarushia bombshell Weusi. “Yo Mchomvu wape salam ‘Kubumkubum’ waimbie watakufa njaa muziki umebadilika,” anarap Nay. Nay pia amemdiss Zitto Kabwe kwa kurap:    “Word up Diamond, mwanangu wewe si mtoto wa Kigoma, mpe

BARNABA SABABU ZILIZOMFANYA KUTEMANA NA SHILOLE

Image
Baada  ya   siku  nyingi  kupita  tangu  Shilole  na  Barnaba  watemane,imebainika  kuwepo  kwa  siri  kubwa   zilisababisha  wawili  hao  watemane .... Chanzo  cha  karibu  na  Barnaba  kimedai  kuwa  sababu  zilizosababisha  wawili  hao  kutemana   ni  pale  shilole  alipodanganya  umri  wake  na  kumwachia  Barnaba  jukumu  la  kumlelea  watoto  wake... "Suala  la  kulea  watoto  wasio  wa  kwake  lilikuwa  ni  gumu  sana   kwa  Barnaba  kwani  wakati  huo  ndo  kwanza  alikuwa anaanza  maisha na  hakuwa  na uwezo  wa  kumhudumia  mtu  na  wanae" ..Kilisema  chanzo  hicho. Chanzo  hicho  kiliendelea  kufunguka  kuwa  Shilole  ndiye  aliye  mtongoza  Barnaba   kwa  staili  ya  kumdanganya  umri  huku  akimweleza  kuwa  swala  la  watoto  wake  lilikuwa  linasimamiwa  na  baba  yao. Habari  zinadai  kwamba, baada  ya  Barnaba  kuingizwa  mkenge, penzi  lao  lilikuwa  kwa  kasi  sana  huku  Shilole  akijitahidi  kuuficha  ukweli  kwa  muda  mrefu.