MAN UTD KUPOTEZA MWELEKEO

Wachezaji wa Man United
Wachezaji wa Man United
kwa mara nyingine tena Manchester United imeandikisha matokeo mabaya kwa kutoka sare nyumbani.
Goli lililofngwa na nahodha Adam Lallana dakika moja kabla ya mechi kumalizika,limeiwezesha Southampton kuondoka na alama 1 kwenye uwanja wa Old Trafford.

Manchester United imepata goli la kuongoza katika dakika ya 25 ya mchezo.
Matokeo hayo ya goli 1-1 ni ya kuvunja moyo kwa mashabiki wa Manchester United ambayo imekwisha funga mechi 2 tu miongoni mwa mechi 7 na sasa iko nyuma ya viongozi wa ligi Arsenal kwa alama 8.
Katika matokeo mengine ya mechi zilizochezwa,Chelsea waliinyuka Cardiff magoli 4-1;Everton ikailaza Hull 2-1;Swansea iliichapa Sunderland 4-0 Stoke wakatoka sare bila kufungana na West Brom.

Comments

Popular posts from this blog

TUMIA SMS HIZI KUBORESHA PENZI LENU

FAIDA TISA ZA MBEGU ZA MABOGA KATIKA MWILI WA BINADAMU

NINI MAANA YA MAPENZI