MBEYA CITY KUITIKISA NCHI KWA SAA KADHAA LEO?, WAWATETEMESHA JKT RUVU SOKOINE, MAKATA AWATULIZA MZUKA!!
“Tunataka kuwaambia Watanzania kuwa klabu yetu ni mpya na ina falsafa mpya kabisa, vijana ndio msingi wetu. Pia tunajua mashabiki ni mchezaji wa 12, tunawaomba wajitokeza leo kwa wingi kwani tutawapa raha kama tulivyofanya huko nyuma”. Alisema Maka.
WAKALI
wapya wa ligi kuu soka Tanzania bara `Nyuki wa nyanda za juu kusini`,
klabu ya Mbeya City wametamba kuwa leo wanataka kuisimamisha nchi kwa
muda na kuwajulisha watanzania kuwa falsafa yao mpya na mtazamo mpya
kweli unafanya kazi.
Akizungumza kwa njia ya simu kutoka jijini Mbeya na mtandao wa Samwelmlawa
muda mfupi uliopita, Kocha msaidizi wa klabu hiyo, Maka Mwalwisyi
amesema wachezaji wote wana morali kubwa na wanategemea kuiambia
Tanzania kuwa falsafa mpya imekuja na watapa matokeo mazuri jioni ya leo
dhidi ya JKT Ruvu na kuongoza ligi kwa saa kadhaa.
“Falsafa
na mtazamo mpya ndio dira yetu, sisi tunaamini kuwatumia vijana wadogo,
tunawafundisha na kuwakumbusha vipaji vyao, watu wengi wanajua ni nguvu
ya soda, lakini watashanga tulivyoanza ndivyo tutakavyomaliza”. Alisema
Maka.
Mbeya
City, `Nyuki wa nyanda za juu kusini` wanaendelea na mpango wao wa
kuwatoa watu nishai, na leo hii kibaruani na JKT Ruvu uwanja wa Sokoine
Maka
alisema wanawaheshimu sana JKT Ruvu kwani wana mwalimu mzuri aliyefanya
kazi
Mbeya, hivyo wanauchukulia kwa umuhimu mkubwa mchezo huo ambao wakishinda watafikisha alama 20 na kama Azam fc atafungwa au kutoa sare leo hii jijini Arusha dhidi ya JKT Oljoro, basi Mbeya City watapanda kileleni wakisubiri matokeo ya kesho Simba na Yanga uwanja wa Taifa.
Mbeya, hivyo wanauchukulia kwa umuhimu mkubwa mchezo huo ambao wakishinda watafikisha alama 20 na kama Azam fc atafungwa au kutoa sare leo hii jijini Arusha dhidi ya JKT Oljoro, basi Mbeya City watapanda kileleni wakisubiri matokeo ya kesho Simba na Yanga uwanja wa Taifa.
Kwa
upande wa kocha mkuu wa JKT Ruvu, Mbwana Makata amesema anajua mchezo
utakuwa ni mgumu, na anajua City wanawaza kivyao na wao kivyao, lakini
wasitegemee mtelemko kabisa kutokana na mazoezi waliyofanya kujiandaa
kuwakabili.
“Wachezaji
wangu wako vizuri na tunategemea kufanya vizuri, ni kweli tumeteteleka
kidogo kwa mechi za nyuma, lakini cha msingi ni kuelewa kuwa ligi ni
ngumu na kuna changamoto nyingi za kiushindani, hivyo mashabiki wasikate
tamaa”. Alisema Makata.
Hata
hivyo tangu ligi imeanza, Mbeya City walishinda mechi moja tu dhidi ya
Ruvu Shooting (mabao 2-1) kati ya nne walizocheza katika uwanja wao wa
nyumbani wa kumbukumbu ya Sokoine.
Walianza
kwa suluhu dhidi ya Kagera Sugar, wakatoka sare ya 1-1 na Yanga,
wakashinda 2-1 dhidi ya Ruvu Shooting,na wakatoa sare ya 1-1 na Coastal
Union, kabla ya kusafiri kwenda nje.
Ugenini
walianzia Manungu ambako walitoka suluhu dhidi ya Mtibwa Sugar,
wakatoka 2-2 dhidi ya Simba SC uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam,
wakashinda 2-1 Sh. Amri Abeid Arusha dhidi ya JKT Oljoro, wakasafiri
mpaka Tabora na kuwafunga Rhino Rangers mabao 3-1 na wakamalizia Tanga
ambapo waliwafunga Mgambo JKT bao 1-0, na hatimaye leo wamerejea tena
nyumbani dhidi ya JKT Ruvu.
Kwasasa
City wapo nafasi ya tatu wakiwa na pointi 17 sawa na Azam fc ambao wako
nafasi ya pili, lakini wana wastani mzuri wa mabao ya kufunga na
kufungwa, na juu yao yupo Simba mwenye pointi 18.
Mechi
nyingine zitakuwa kati ya Oljoro JKT na Azam (Uwanja wa Sheikh Kaluta
Amri Abeid, Arusha), Mtibwa Sugar na Mgambo Shooting (Uwanja wa Manungu,
Turiani), Ashanti United na Ruvu Shooting (Azam Complex Chamazi, Dar es
Salaam) na Kagera Sugar dhidi ya Coastal Union (Uwanja wa Kaitaba mjini
Bukoba).
Wakati
huo huo, Ligi Daraja la Kwanza (FDL) nayo inaendelea katika viwanja
nane leo (Oktoba 19 mwaka huu) huku Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar
es Salaam ukiwa mwenyeji wa mchezo kati ya African Lyon na Friends
Rangers.
Nayo
Villa Squad itacheza na Green Warriors katika Uwanja wa Mabatini,
Mlandizi, Polisi Morogoro na Kimondo (Uwanja wa Jamhuri, Morogoro),
Lipuli na Kurugenzi (Uwanja wa Kumbukumbu ya Samora mjini Iringa) na
Mkamba Rangers dhidi ya Majimaji (Uwanja wa CCM Mkamba, Morogoro).
Toto
Africans na Mwadui (Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza), Polisi Dodoma na
Polisi Tabora (Uwanja wa Jamhuri, Dodoma), wakati Polisi Mara na pamba
zitacheza kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume mjini Musoma.
Comments
Post a Comment