Moyes awaomba subra mashabiki

Kocha mpya wa Man U David Moyes
Kocha wa Manchester United David Moyes amewaonya mashabiki wa mabingwa wa ligi kuu ya England kwamba anahitaji kuimarisha kikosi chake na kwamba kipigo cha Jumaapili ambapo walichapwa 4-1 na Manchester City huenda isiwe ndio mwisho wa matokeo kama hayo.
"kutatokea siku kama ile ya Jumaapili na huenda tukakabiliwa na matokeo zaidi kama hayo kwa sababu tuko katika kipindi cha mpito," alwaaambia waandishi habari kabla ya pambano la Jumaatano la kombe la Capital One dhidi ya Liverpool...

"bado tunakabiliwa na kazi pevu ya kuwasajili wachezaji sio tu watakaojumuishwa na kikosi chetu lakini wenye uwezo wa kuingia moja kwa moja katika timu," aliongeza kusema Moyes katika msimu wake wa kwanza katyika a Old Trafford baada ya kushikikilia nafasi iliyoachwa na Alex Ferguson.
"tulihitaji wachezaji wawili watatu hivi ambao wangeweza kuingia moja kwa mopja katika timu. Lakini hayo yatatokea ,kweli huenda itabidi nikabiliane na vipigo vichache zaidi.
Manchester United iliwakosa wachezaji kadhaa mashuhuri wakati wa kipindi kilichopita cha usajili na hata kulikua na tetesi za juhudi za dakika ya mwisho za kuipiku Real Madrid ili kumsajili Gareth Bale ambae kuuzwa kwake kutoka Tottenham Hotspur kulivunja rekodi kama mchezaji ghali kupita wote duniani.
Juhudi za kuwasajili Cesc Fabregas kutoka Barcelona, Ander Herrera kutoka Athletic Bilbao na Fabio Coentrao kutoka Real Madrid ziliambulia patupu.
Leighton Baines aliamua kubaki Everton wakati Thiago Alcantara aliamua kuihama Barcelona na kujiunga na Bayern Munich.
Moyes badala yake alikimbilia kumsajili mchezaji wa kiungo wa Ubelgiji Marouane Fellaini, kutoka klabu yake ya zamani Everton, kwa dola millioni ($43.96 ) dakika chache tu kabla ya kufungwa dirisha la usajili.

Comments

Popular posts from this blog

TUMIA SMS HIZI KUBORESHA PENZI LENU

FAIDA TISA ZA MBEGU ZA MABOGA KATIKA MWILI WA BINADAMU

NINI MAANA YA MAPENZI