MOURINHO VICHAPO, MAN UNITED NA NYIMBO, WENGER NA BUTwAA KWA RAMSEY!!


WENGER_ASHANGAA 













KLABU Vigogo huko England, Mabingwa Manchester United, Chelsea na Arsenal, hivi sasa zinapitia kwenye nyakati tofauti huku Stamford Bridge ikikaribisha vichapo mfululizo, Old Trafford wakibuni mbinu mpya za kuhamasisha ushindi kwa kutenga Jukwaa maalum la Waimbaji na huko Emirates Meneja Arsene Wenger amshangaa Mchezaji wake Aaaron Ramsey....
MOURINHO NA KICHAPO
Jose Mourinho amekubali kuwa kipigo cha 2-1 walichoshushiwa na FC Basel Jana Usiku kwenye Mechi ya UEFA CHAMPIONS LIGI, UCL,  ni jukumu lake analopaswa kuwajibika na pia kukiri kuwa kichapo hicho ni hatua moja nyuma kwao.
Hicho ni kipigo cha pili mfululizo kwa Chelsea baada ya Wikiendi pia kufungwa Bao 1-0 na Everton katika Mechi ya Ligi Kuu England.
Na Mourinho amesema: “Mimi ndie Meneja. Mimi ndie mwenye jukumu la kila kitu. Hasa baada ya matokeo mabaya. Katika wakati mzuri nataka kila Mtu ang’are na wakati mbaya kila Mtu atulie. Kesho nitaamka bila tabasamu usoni lakini Saa 1 Asubuhi nitaanza kufanya kazi kwa bidii kusaka Pointi 3 kwa Fulham. Mechi ijayo tunakwenda Bucharest na lazima tupate Pointi ili turudi kwenye UCL. Hatutaki kucheza EUROPA LIGI!”
MAN UNITED NA NYIMBO
Manchester United watafanya majaribio Uwanjani Old Trafford kwenye Mechi ya UCL dhidi ya Real Sociedad kwa kuweka eneo moja la Jukwaa kuwa sehemu maalum ya Washabiki ambao watakuwa wakiimba Nyimbo za kuhamasisha.OLD_TRAFFORDbest
Mpango huu ulitaka kujaribiwa Siku za nyuma lakini ukapingwa na Polisi kwa vile eneo la Jukwaa lilopangwa kuwaweka Waimbaji lilikuwa ni maalum kwa Washabiki wa Timu za Upinzani na ilibidi Mashabiki hao wahamishwe na kuwekwa kwenye Jukwaa jingine nyuma ya Maeneo ya Mabenchi ya Ufundi wa Timu kitu ambacho Polisi walikiona ni hatari.
Lakini safari hii Klabu imeunga mkono ombi la Mashabiki wao wa kuwa na Jukwaa la Waimbaji ili kuongeza sauti katika kuhamasisha Timu yao kwenye Mechi.
Inatarajiwa eneo hilo maalum la Jukwaa kwa ajili ya Waimbaji litakuwa na Washabiki 1,400 kwenye upande wa Kusini Mashariki hapo Oktoba 23 wakati wa Mechi na Real Sociedad.
Nae Kiungo wa Man United, Michael Carrick, ameunga mkono hatua hii kwa kutoa kwenye Akaunti yake ya Twitter posti: “Ni wazo zuri sana kuwa na eneo la Waimbaji. Kama ningekuwa naenda kama Shabiki hapo ndio ningetaka niwe….!!”
WENGER NA BUTAA KWA RAMSEY!
Bosi wa Arsenal Arsene Wenger amesema ufungaji Magoli wa Aaron Ramsey kwa sasa ni kitu kinachoshangaza.
Jana Usiku, Ramsey alifunga Bao moja wakati Arsenal wanaichapa Marseille 2-1 katika Mechi ya UCL na hilo ni Bao lake la 6 Msimu huu.
Wenger amekiri: “Hakika sikutegemea yeye kufunga Bao nyingi namna hii lakini ameonyesha kuongezeka ubora wake katika pasi zake na kiwango cha ufundi. Hilo ni muhimu kwani mara nyingi huchomoza sehemu muhimu kwenye eneo la Penati.”
++++++++++++++++++++++
Ramsey apiga 6 Msimu huu:
18 Septemba: Bao moja dhidi ya Marseille, ushindi wa in 2-1
14 Septemba: Goli 2 walipoifunga Sunderland 3-1
27 Agosti: Goli 2 Mechi ya Marudiano na Fenerbahce kwenye UCL
21 Agosti: Goli 1 walipoifunga Fenerbahce Mechi ya Kwanza ya UCL
++++++++++++++++++++++
Wenger aliongeza "Kufunga Mabao kunatokea kwa mzunguko na kitu muhimu ni ubora wake kimchezo."
Mwaka 2010 Ramsey, mwenye Miaka 22, alivunjwa Mguu sehemu mbili na Beki wa Stoke City Ryan Shawcross na kukaa nje ya Uwanja kwa Miezi 9.
Jumamosi Arsenal watacheza Uwanjani kwao Emirates na Stoke City kwenye Mechi ya Ligi.

Comments

Popular posts from this blog

TUMIA SMS HIZI KUBORESHA PENZI LENU

FAIDA TISA ZA MBEGU ZA MABOGA KATIKA MWILI WA BINADAMU

NINI MAANA YA MAPENZI