KOCHA KIM PAULSEN WA TAIFA STAR AFUNGUKA NA MECHI YA GAMBIA SEPT 7 2013
Stars
 ambayo ilianza vema michuano hiyo na kuweka hai matumaini ya kufuzu 
kushiriki fainali za kombe la dunia zitakazochezwa mwakani nchini Brazil
 kabla ya kupoteza mechi mbili dhidi ya Morroco ugenini na dhidi ya 
Ivory Coast hapa nyumbani na kujikuta ikiangukia katika nafasi ya tatu 
kwenye kundi lake linaloongozwa na tembo wa Ivory ccast na kufuatiwa na 
Morrocco huku Gambia ikikamata mkia.
Akizungumza
 kwenye kambi ya timu hiyo jijini dar es salaam  Kim Paulsen amesema 
baada ya kupoteza nafasi ya kusonga mbele kwenye michuano ya kufuzu 
kombe la dunia sasa amejikita katika kutengeneza kikosi imara kwa ajili 
ya mashindano ya kufuzu fainali za afrika . Hata hivyo katika mchezo huo
 dhidi ya Gambia Kim atalazimika kuwakosa nyota wake wanne kutokana na 
kuwa majeruhi ambao ni Kelvin Yondani, Athumani Idd Chuji, Shomari 
Kapombe na John Boko 'adebayo'
Stars
 imeingia kambini tangu septemba 29 kujiandaa na mchezo huo na imekuwa 
ikifanya mazoezi katika uwanja wa kumbukumbu ya Karume na uwanja wa 
taifa ambapo wachezaji wa kimataifa wa tanzania wanaokipiga katika klabi
 ya TP Mazembe ya DRC Thomas Ulimwengu na Mbwana Samata wanatarajia 
kujiunga na wenzao kambini katikati ya wiki hii tayari kwa safari ya 
kwenda Gambia.
 
Comments
Post a Comment