SUALA LA PAPIC, YANGA LASUBIRI UAMUZI WA FIFA!!
Shirikisho
 la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limewasilisha rasmi suala la 
madai ya aliyekuwa Kocha wa Yanga, Kostadin Papic dhidi ya klabu hiyo 
katika Kamati ya Hadhi ya Wachezaji.
FIFA
 imesema imepeleka rasmi suala hilo katika kamati yake hiyo baada ya 
kupokea vielelezo vya Papic anayedai kuidai Yanga dola 10,000 za 
Marekani pamoja na vile vya Yanga inayodai kumlipa kocha huyo fedha zote
 alizokuwa akiidai klabu hiyo.
Kwa
 taratibu za FIFA, hivi sasa haitapokea vielelezo vingine kutoka pande 
hizo mbili, na badala yake Kamati hiyo inayoongozwa na Theo Zwanziger 
kutoka Ujerumani itafanya uamuzi na kuziarifu pande husika. Zwanziger 
kitaaluma ni mwanasheria.
Papic
 aliyeinoa Yanga kwa vipindi viwili tofauti aliwasilisha malalamiko yake
 FIFA akidai hadi mkataba wake unamalizika klabu hiyo ilikuwa haijamlipa
 dola 10,000 za Marekani.
 
Comments
Post a Comment